This post is from a suggested group
SANTURI – Sauti ya Ukweli wa Maisha

Kuna kitu watu wengi hawakikubali… Sio kila anayekaa kimya ana amani. Wengine wananyamaza kwa sababu wamechoka kuelezea wanavyo jisikia. Unakuta mtu alikuwa anajitahidi kuongea, kueleza maumivu yake, kueleza anacho pitia… lakini hakusikilizwa. Sasa ameacha kuongea, si kwa sababu hana la kusema, bali ameona hakuna anayemuelewa.
Ukiona mtu amenyamaza sana, usikimbilie kusema ana kiburi.Inawezekana amechoka kupuuzwa. Inawezekana amejeruhiwa mara nyingi mpaka ameona ukimya ni salama zaidi kuliko maneno. Maisha yanahitaji kitu kimoja ambacho wengi wanakikosa — kusikiliza kwa moyo, sio kwa masikio tu.
Leo jaribu kitu kidogo: Msikilize mtu wako wa karibu bila kumkatiza… bila kumhukumu… bila kumpa majibu ya haraka. Wakati mwingine mtu hahitaji suluhisho… anahitaji tu ajisikie anaeleweka.
Swali la leo: Je, wewe huwa unasikiliza kuelewa… au unasikiliza kujibu?— SANTURI








